Christian Bella awaacha mashabiki wa kimara njia panda

Mwanamuziki Christian Bella, wikiendi iliyopita alisababisha taharuki ya aina yake baada ya kutoonekana katika shoo iliyopangwa kufanyika kwenye Ukumbi wa White House uliopo Korogwe Kimara jijini Dar es Salaam.



Mashabiki wa bendi ya Malaika walifurika hadi ukumbi kutapika wakiwa na usongo wa kumwona na kusikia sauti ya Bella ambaye kwa sasa anavuma na wimbo wa Nani Kama Mama.

Tofauti na matarajio yao, mashabiki hao hadi usiku mnene hawakumwona msanii huyo ambaye inadaiwa hayupo nchini na kwamba waandaaji waliamua kuwatapeli fedha zao. Kiingilio kilikuwa Sh 10,000.

Baada ya kukata tamaa ya kumwona Bella ndipo ghasia zilipoanza kwa mashabiki hao wanaodaiwa kujawa na hasira kuanza kuvunja meza na kurusha viti na chupa za bia jukwaani na hivyo kuwa hitimisho la shoo hiyo.
Previous Post Next Post